Friday, 17 February 2017

FAIDA ZA KUFANYA MAZOEZI



Imeandikwa na Julius I.Sanare
0757- 012317
www.blogger.com au www.jitambue1.blogspot.com
FAIDA ZA KUFANYA MAZOEZI
Moja ya mahitaji muhimu kwa mwanadamu ni Mazoezi. Mazoezi ni mhimu kwa ajili ya afya pamoja na kuwa na maumbile ya kuvutia (sex body).Watu wengi huishia kula chakula tu bila kufanya mazoezi, hata kama utakula vizuri vipi bila mazoezi mlo haujakamilika. Kwa hiyo mazoezi ni muhimu kama ilivyo kwa maji na chakula katika miili yetu.
Zifuatazo ni faida za kufanya mazoezi.
Ø  Hukufanya ujisikie vizuri
Ø   Huongeza uwezo wa kujifunza
Ø   Hujenga uwezo wa kujistahi
Ø  Huongeza nguvu ya ubongo kufanya kazi
Ø   Huuweka mwili wako kuwa unaofaa (fit) na wenye uwezo
Ø   Huongeza afya ya akili yako
Ø   Huongeza kinga ya mwili
Ø   Hupunguza mfadhaiko/stress
Ø  Hukufanya ujisikie vizuri/mwenye furaha
Ø   Hukufanya usizeeke mapema
Ø   Huweka ngozi yenye mng’aro na yenye afya
Ø  Husaidia kupata usingizi mtulivu
Ø   Husaidia kuzuia ugonjwa wa kiharusi/strokes
Ø   Huongeza ufanisi katika makutano/joints za mwili
Ø  Huongeza nguvu za mishipa
Ø   Huondoa wasiwasi
Ø   Huongeza kumbukumbu
Ø   Husaidia kudhibiti ulevi/uteja
Ø   Huongeza uzalishaji
Ø  Huongeza uwezo wa ubunifu
Ø  Hupendezesha muonekano wa mwili
Ø   Huongeza uwezo wa kujiamini
Ø   Husaidia kuongeza nguvu juu ya malengo yako maishani
Ø   Huondoa tatizo la kukinaishwa na chakula
Ø   Huongeza miaka ya kuishi
Ø   Hukomaza mifupa
Ø   Huongeza afya ya moyo
Ø  Huongeza hali ya kuwa na msimamo
Ø  Huondoa homa ndogo ndogo mwilini
Ø   Huongeza hamu ya kula
Ø  Hupunguza uwezekano wa kupatwa na baadhi ya kansa
Ø  Hushusha shinikizo la juu la damu
Ø   Hupunguza uwezekano wa kupatwa na kisukari
Ø  Huzuia kupatwa na ukichaa/uwendawazimu
Ø   Hupunguza au huzuia maumivu ya mgongo
Ø  Hupunguza uwezekano wa kupatwa na ugonjwa wa mifupa
Ø  Hupunguza hisiaaufikra za kujisikia vibaya au huzuni
Ø  Huzuia kupotea kwa mishipa
Ø  Huongeza nguvu na ustahimilivu
Ø  Huongeza ufanisi katika michezo
Ø   Huongeza uwezo wa kuvumilia maumivu
Ø   Huongeza usawa na ushirikiano wa mwili
Ø  Huongeza usambazaji wa oksijeni katika seli za mwili
Ø   Huongeza hali ya ufuatiliaji
Ø   Huongeza uwezo wa kujitawala na kujidhibiti nafsi
Ø   Huondoa uchovu
Ø   Huongeza nguvu katika tendo la ndoa
Ø   Hufanya maisha yawe kuvutia zaidi
Ø  Huongeza ubora wa maisha
Tujitahidi sana kufanya mazoezi kwani yatatusaidia sana katika kujenga miili yetu.

No comments:

Post a Comment